Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Saturday 16 February 2013

KIM KARDASHIAN ATUA NIGERIA, AUZA MJENGO WAKE!


The reality Tv star Kim Kardashian ametua nchini Nigeria saa moja lililopita. Kim K anayetarajia mtoto wake wa kwanza na rapper Kanye West yupo Nigeria kwa ajili ya ku co-host concert iitwayo ‘Love Like A Movie” ya Darey Art Alade, itakayofanyika kesho tarehe 17 February huko Eko Hotel Convention Center.


Kim alitua airport akiwa na bodyguard wake pamoja na makeup artiste
Wakati huohuo Kim ameuza mjengo wake uliomgharimu dola milioni 4.8 aliununua mwaka 2010. Inasemekana ameuuza kwa chini ya bei hiyo pamoja na samani za ndani kama makochi. Mjengo aliouuza alikuwa akiutumia yeye na x-boy friend wake, Kris Humphrey! 




Nje mpaka ndani ya mjengo alioupiga bei KK

DRAKE AZUIWA KUINGIA CLUB SABABU YA CHRIS BROWN!


Chris Brown na Drake sasa hawapikiki chungu kimoja! Usiku wa Jumatano Drake alizuiwa kuingia club moja sababu Chris Brown alikuwa tayari ndani!

Mabaunsa waliokuwa mlangoni klabuni Playhouse huko Hollywood walimkatalia katakata Drake kuzama ndani kula bata na wanae vile CB alikuwa tayari akila bata na washkaji zake katika party ya kampuni ya mavazi ya ‘Popular Demand’.
 
Mabaunsa walijuafika kuwa kama Drake angeingia ndani basi pengine kingetokea kilekile kilichotoka W.i.P. nightclub. Unakikumbuka? Majamaa walitupiana vyupa sana na kusababisa uharibika wakutosha!

Ki-gentleman, Drake alisepa zake kimyakimya bila kubishi!


EXCLUSIVE: MAPYA YA MAREHEMU GOLDIE: MUME WAKE AIBUKA NA USHAHIDI KIBAO WA PICHA ZA HARUSI YAO!















EXCLUSIVE: MUME WA GOLDIE AIBUKA, AMPIGA BITI PREZZO!


Nobody knew bout this! Kumbe Goldie Harvey, mshiriki wa BBA stargame alikuwa ameolewa kabla hajafa! Andrew Harvey, raia wa Uingereza ameibuka na picha zote za harusi yao waliofunga kwa siri nyingine kibao wakati wakila bata pamoja.

Andrew na Goldie Harvey
Andrew na Goldie Harvey batani.
Andrew Harvey ameongeza kuwa yeye na Goldie walikuwa bado katika mahusiano na mawasiliano mazuri mpaka umauti ulipomfika. Andrew alikutana na Goldie katika party ya rafiki yake huko Lagos. Ndipo mfanyabiashara huyo wa mafuta akafunga ndoa na Goldie, December, 2005. Pia Andrew amekana marehemu Goldie kuhusishwa na matumizi yaliopitiliza ya madawa ya kulevya kuwa ndio moja ya sababu za kifo chake!


Upande mwingine pia Andrew Harvey alimpiga biti Prezzo na kumtaka kutojihusisha kabisa na maswala yoyote ya Goldie. Prezzo na Goldie walikuwa wakutane Lagos tarehe 15 February kwa ajili ya kusherehekea Valentine’s. 

Prezzo na Goldie mjengoni BBA



AKON MADENI TUPU!


Akiwa na idea ya kuanzisha website kwa ajili ya artistes mbalimbali ku-interact na fans wao, matokeo yake ni kusimama kizimbani! Akon, ‘Lonely’ singer, amefunguliwa mashtaka na kampuni ya Atlanta Business Video huko Georgia wakilalamika kuwa Akon aliwaajiri mwaka 2011 kwa kazi ya kuitengeneza site yake lakini hawajaambulia chochote.

Atlanta Business Video waliajiriwa na Akon kuiboresha “Fantrace” na kuifanya kuwa website rasmi. Kwa taarifa yako tu, “Fantrace” ilikuwa facebook forum iliyokutanisha wasanii na raia, idea ya Akon na kutengenezwa na makampuni mawili.

Atlanta Business Video waliitwa baadae na Akon ili kuiboresha na kuifanya sasa iwe website. Hapo ndipo ABV wakaingia mzigoni na kufanya kazi kwa masaa 1,023 ambapo Akon alitakiwa awalipe dola 127,875, ambazo mpaka leo Akon hajawalipa hata sumni! 

Akon