Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Monday 11 March 2013

MARIAH CAREY IS BACK TO THE GAME!

Kwa zaidi ya miaka miwili sasa Mariah Carey alifokas zaidi kulea watoto wake na pia kuwa jaji katika shindano la American Idol! Na sasa the diva herself is back to the business to the fullest! Mtoko mpya unaitwa 'Almost Home'. Ngoma hii pia imetumika kama soundtruck ya movie mpya, 'Wizard Of Oz'.


Albam ya mwisho ya Mariah ni 'Memoirs Of An Imperfect Angel' na ilitoka mwaka 2009. Carey, 42,  amekuwa bize sana kwa mazoezi na shughuli nzima ya kurekodi albam hii! 



Mariah Carey ameshaachia baadhi ya vipande (picha) vya ngoma hiyo na vinapatika hapa tu kwa sasa!


 


JUSTIN BIEBER AFUTA SHOW URENO!

Ni kama vile Justin Bieber amesanukia mchongo hivi na fasta kwa kushirikiana na waandaaji wa show yake wakaamua kuifutilia mbali show yake. Show ilikuwa ipigwe huko Ureno. Kimsingi JB alikuwa agonge shows mbili, moja tarehe 11 na nyingine tarehe 12 March. Sasa ya tarehe 12 ndio iliyopigwa chini na raia wote walionunua tiketi za show hiyo watarudishiwa mkwanja wao!


Habari toka katika mtandao wa ukumbi aliotakiwa JB kupiga show zinasema kuwa ni sababu za kibiashara zaidi ndio zilizofanya kufutwa kwa show hiyo.  Inasemekana Justin Bieber anahofia kupigia show viti kutokana na yale yaliyotokea katika concert yake huko London ambako alichelewa kwa zaidi ya dakika 45 na kuwaudhi mashabiki wake hivyo wengi wao kusepa hata kabla Bieber haja-perform!  

Ni asilimia 60 tu ya tiketi za show hiyo ya March 12 ndio zilikuwa zimeuzwa.

O2 Arena London, Justin Bieber alipiga show huku yiti vingi vikiwa vitupu!