Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Saturday 13 April 2013

PAUL WA P-SQUARE APATA MTOTO!

Baada ya pacha wake Peter kupata mtoto wa pili wa kike sasa ni zamu ya Paul. Jana Paul Okoye na mchumba wake wa muda mrefu Anita, walipata mtoto wao wa kwanza wa kiume. Mtoto huyo aliyepewa jina la Andre alizaliwa Atlanta, USA.

Peter tayari ana watoto wawili, toka kwa demu wake wa muda mrefu Lola Omotayo. Welcome to the world Andre Okoye.




SIZE 8: KUKAA UCHI BASI!

Baada ya msanii wa kike Size 8 kutangaza jana kuokoka, sababu ya haraka haikujulikana mapaka alipofanya interview na kutoa yale yaliokuwa yanamsibu. Size 8 ambae kuna wakati nchini Kenya alitangazwa kama msanii mwenye mkwanja mrefu kuliko wote alisema kuwa moja kati ya sababu za yeye kuokoka na kuacha mziki wa kidunia ni pale alipokuwa akitoka kupiga shows za usiku huwa analia usiku mzima na moyoni hakuwa akijisikia amani.


Pia Size 8 alisema kuwa kufuatia hali hiyo ya kutosikia amani moyoni mwake aliamua hata kuipiga chini show ambayo ilikuwa imuingizie milioni 2 za Kenya. Alipoulizwa kama ataendelea kuvaa vimini-vichupi na vinguo vifupi alivyokuwa akitupia hapo awali, Size 8 alisema, "hizo sasa zimekuwa mbaya. No more! No more skimpy clothing! Unajua hizo mavazi zinatisha watu. Sasa nitakuwa nikivaa mavazi za heshima. Mavazi zenye Jehovah pia anafurahia akiniona nazo. Si lazima ikuwe dress refu. Nguo tu ya heshima."


Size 8 tayari ameshatoa ngoma ya gospel iitwayo 'Mateke', icheki hapa:-



P-SQUARE WATOA ONYO!

Kupitia internet biashara kwa wasanii huko Naija imekuwa ngumu sana baada ya kujitokeza makundi ya watu kadhaa wakifanya wao ni mapromota hivyo kuchukua advance za wasanii mbalimbali huku wasanii wenyewe wakiwa hawajui lolote! Mwaka jana kuna mtu alilamba dola 100,000/= kupitia twitter na facebook kwa kudai kuwa yeye ni promota wa kundi la P-Square nchini Ufaransa.

P-Square wametoa onyo kwa wale watakaotaka kuingia nao mikataba ya show kwa kuwa makini na watu hawa katika mitandao hii ya kijamii! Kupitia akaunti yake ya twitter, Peter Okoye alitoa onyo kwa kuandika:
  

Kwa sasa P-Square ndio wasanii wanaolipwa mkwanja mrefu zaidi nchini Nigeria kwa kuchaji dola 150,000/= kwa shows za kimataifa na Naila milioni 10 kwa shows za nyumbani kwao Nigeria!