Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Wednesday 27 March 2013

D' BANJ AMTWANGA MAKOFI MANAGER WAKE, AMTIMUA KAZI!

Wiki chache zilizopita, aliyekuwa manager wa Koko Master, Dapo Oyebanjo a.k.a D'banj, Abisagboola Oluseun John aka Bankuli alifukuzwa kazi na kichapo juu! Chanzo cha data hii kinasema kuwa mnamo December mwaka jana baada ya show, 'Koko concert', Bankuli alipaa zake kwenda Paris Ufaransa kuipigia promo album mpya ya Kanye West bila kumpa taarifa D'Banj. Koko Master akampa vitasa/makofi na kumtimua kazi right away!
Bankuli alivunja ukimya na alikuwa ana yake ya kusema,"D’Banj hakunifukuza ila ni uamuzi wangu mwenyewe" Bankuli pia alikana kufanya kazi na Kanye West bila ruhusa ya D' Banj!
Inasemekana D'Banj ni msanii mgumu kum-manage. Anaamua atakacho na ni mgumu kufuata ushauri vile kila mtu anayefanya kazi naye, Baba (D’Banj) mwisho wa siku aliamua kusepa zake!
 
D'Banj na Bankuli
 

GAUNI GHALI ZAIDI DUNIANI!

The saying diamonds are a girl’s best friend has been taken to a whole new level as the world's most expensive dress has been unveiled.




 
Bei yake: £11.7m
Designer: Debbie Wingham
 

Monday 25 March 2013

MWANAMKE MWENYE MIGUU MIREFU ZAIDI DUNIANI!

Ni Svetlana Pankratova. Ni mcheza basketball wa zamani  raia wa Urusi mwenye kimo cha futi 6 na nchi 5 (1.96 m). Miguu yake ina urefu wa futi 4 na nchi 4 (1.32 m)




MTOTO WA MIAKA 8 AOA KIBIBI CHA MIAKA 61!

Dogo wa miaka 8, Sanele Masilela, amefunga ndoa na kibibi cha miaka 61. Dogo huyo ambaye ni mwanafunzi wa Primary school ameushangaza Ulimengu kwa kumuoa ajuza  Helen Shabangu huko Tshwane, South Africa.

Ingawa ndoa hiyo haitambuliki kisheria lakini dogo amekomaa kwa kusema kuwa sasa anajihisi ni mme kamili na ana wajibu kwa ndoa yake akiwa kama mme!

Dogo alifunguka haya katika siku ya ndoa yake na kuwaacha wahudhuriaji wa ndo hiyo vinywa wazi, "Leo ni siku kubwa kwetu (mimi na mke wangu) kama vile nilivyoitarajia. Marafiki zangu walifikiri na wanaona ni vichekesho nilipofunga ndoa hii lakini mimi najiona ni mwenye furaha na kujihisi kama mme kamili sasa"

Bwana Sanele Masilela na Bi. Harusi Helen Shabangu

Bwana na Bi Harusi wakipata chakula cha usiku!













HAIHUU!!

Mwanamuziki wa Marekani Nicki Minaj alinaswa na kamera akiwa nyuma ya gari lake aina ya Maybach akiwa ameuchapa 'fofofo' huku mguu mmoja ukiwa Magharibi na mwingine Mashariki ya mbali!



Thursday 21 March 2013

MASTAA WALIOREKEBISHA VINYWA VYAO

Hawa ni baadhi ya mastaa waliorekebisha vinywa vyao kwa kufanya operesheni na kufanya meno yao kupangika vizuri hivyo midomo yao kupata taswira nzuri!

1. Celine Dion

 2. Keyshia Cole
  
3. Ludacris

4. Mike Tyson


5. Nichola Cage 

6. Cheryl Cole



1.

Tuesday 19 March 2013

OBAMA AFANANISHWA NA SHETANI!

Kupitia kituo cha television cha History Channel, tamthiliya ya "The Bible" inayoonyeshwa kupitia channel hiyo imekuwa gumzo kutokana na 'shetani' anayeonekana katika movie hiyo kufanana na rais wa 44 wa Marekani, Barack Obama. 
 
Tamthiliya hii ya kidini imetengenezwa na Mark Burnett na kuchezwa na Mehdi Ouzaani imevuta hisia za watazamaji wengi na kwa kuonekana kwake siku ya Jumatano iliyopita imeweza kutazamwa na watazamaji milioni 13.1

















MWONEKANO WA AMBER ROSE BAADA YA KUJIFUNGUA!

Kwa kipindi cha takribani mwezi mmoja Amber Rose alikuwa very busy akimlea mtoto wake Sebastian. Sasa A.Rose anaweza hata kuchat katika mitandao ya kijamii na fans wake, kushare pics na hata kutoka nje for shopping.




Amber rose na mama yake wakifanya shopping


D' BANJ AJA NA DOCUMENTARY!

From Lagos to France to New York, Koko master, D' Banj anakuja na documentary ya dakika 90 inayohusu hustle zake za kimuziki. Interviews za radio na tv, performances mbalibali na maisha yake ya kimuziki kwa ujumla yamewekwa katika doc hii inayoitwa "The Tales of Oliver Twist - The Documentary". The Boss himself Kanye West pia ametokelezea katika doc hii!

Chungulia hapa Documentary hiyo:

















LIL WAYNE ATOKA HOSPITALI!

Hatimaye 'Mirror' hitmaker Lil Wayne ameruhusiwa kutoka hospitalini, California's Cedars-Sinai Medical Center's intensive care unit (ICU) alikokuwa amelazwa kwa siku 6 zilizopita. Lil Wayne a.k.a Dwayne Carter alipatwa maswahibu hayo baada ya kubugia madawa ya kulevya aina ya 'codeine' kupitiliza mpaka kupoteza fahamu kabisa.

Young Money president Mack Maine alithibitisha kutolewa kwa Wayne kupitia akaunti yake ya twitter, ''Thanks to Cedar Sinai for everything!!! @LilTunechi has been officially been released and is headed home....God is great (sic)''. ''God Bless.my son just release frm hospital.thanks 4 all tha luv.YMCMB.Richgang (sic)''



 




GHARAMA ZA WASANII HAWA KUPIGA SHOW NI NOMA!

Tajiri la kutupwa huko South Afrika,  Vivian Imerman amemchomolea msanii Adele toka Uingereza ku-perform katika harusi ya binti yake, Megan kutokana na gharama za msanii huyo kuwa juu mno. British singer Adele anahitaji pauni milioni 2.5 ili kutua South Africa na kupiga show hiyo. Hii ina maana kuwa kwa dakika 1 Adele anahitaji kulipwa pauni laki 1 na kwa vile show yake ilihitajika kuchukua dakika 25 hivyo ghararma yake ikawa pauni milioni 2.5!

Ikumbukwe miaka 2 iliyopita Taikuni hili lilimlipa Amy Winehouse maelfu ya dolari kwa ajili ya ku-perform katika harusi ya dada yake Megan, Bianca na alitarajia hivyo kwa Adele lakini alishangazwa kwa bei juu aliyoitaka Adele. Lakini dhamara ya  Vivian Imerman iko palepale na sasa anasaka msanii mwingine tofauti na Adele!


Adele
Wasanii wengine pamoja na gharama zao za kupiga show ni kama ifuatavyo:-
1. Jay Z & kanye West - $3,000,000
2. 50 Cent - $2,000,000
3. Eminem - $1,650,000
4. Rihanna - $800,000
5. Lil Wayne -  $500,000
6. Drake - $155,000
7. Nicki Minaj - $150,000
8. Akon - $120,000
9. T.I. - $110,000
10. Snoop Dogg - $105,000

Monday 18 March 2013

SIKU YA 6: LIL WAYNE BADO HAJITAMBUI ICU!

Ni siku ya sita sasa toka Lil Wayne akimbizwe hospitali, L.A.'s Cedars-Sinai hospital akiwa hajitambui. Na bado mpaka sasa yupo ICU akiwa hajitambu. Ni kutokana na utumiaji wa madawa ya kulevya kupindukia. 

Mastaa wakiwemo Drake na Nicki Minaj, Eminem, Birdman na wengine kibao walimiminika hospitali kumjulia hali Wayne. Kitanda cha Lil Wayne kimezungukwa na ndugu jamaa na marafiki wakimwombea afya njema na vilio vimetawala pia hospitalini hapa!

 
Madaktari wanaomtibia Wayne ilibidi wali-flash tumbo lake mara 3 ili kuondoa madawa ya kulevya aina ya 'codeine' baada ya Lil Wayne kubugia madawa hayo kupitiliza!

















P-SQUARE WAISIMAMISHA MALAWI!

The Alingo stars, P-Square wako katika tour yao katika mataifa ya barani Afrika na wik-end iliyokwisha walikuwa nchini Malawi na kuangusha bonge moja la show. Show ilikuwa hivi:








JUMBA BEI GHALI ZAIDI NCHINI UINGEREZA!

Hii ndio nyumba ghali nchini Uingereza. Kutokana na bei yake kuwa juu sana ilibidi ipunguzwe kwa takribani pauni milioni 35. Na hii imechukua miaka miwili bila mnunuzi kupatikana.  Na sasa bei yake ni pauni milioni 65 tu!


Bangaloo hili lina vyumba 14 vya kulala na linapatikana katika mtaa wa Hampstead, mtaa huu unajulikana kama 'Billionaires' row' kwa sababu wakazi wa eneo hilo ni wanauwezo kiuchumi!



 Jumba hili la kifahari lilijengwa mwaka 1910 liliwekwa sokoni toka mwaka 2011 na bei yake ilikuwa ni pauni za Uingereza, milioni 100.






















Sunday 17 March 2013

PETER MSECHU KUZALIWA UPYA KESHO!

Peter Msechu kesho atasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka kadhaa. Peter Msechu ambaye ni Bongo Star Search na Tusker Project Fame Star anatarajia pia ku-release his new hit single hiyo kesho. 

Ngoma hiyo inaitwa 'Kumbe' amemshirikisha 'Mwamba wa Kaskazini', Joh Makin!   

Happy Birthday Peter Msechu.