Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Thursday 18 July 2013

NUKUU YA LEO

DIAMOND ASHIKA NAMBA MOJA AFRIKA MASHARIKI!

Kubali au kataa, mpende au mchukie lakini ukweli utabaki palepale kuwa kwasasa msanii toka Tanzania, Diamond Platnumz a.k.a Naseeb Abdul ndio mwenye nguvu kubwa zaidi katika majukwaa yote ya Afrika Mashariki.



Kwa mujibu wa website moja huko Kenya anayemfuata kwa ni nguli Dk. Jose Chameleone ambaye kwa kipindi kirefu sana ameweza kukusanya raia wengi popote pale anapopiga show hasa East Africa. Achana na Chameleone, Diamond hivi sasa ameonekana kung'arisha zaidi huku makampuni makubwa hasa ya Kitanzania kila leo yakibisha hodi nyumbani kwa Diamond ili kuingia naye mikataba (endorsements).

Moja kati ya vipimo sahihi vya Diamond kuwa juu kwasasa ni ile show ya Congo iliyosababisha foleni ambayo haijawahi tokea huko Congo kutokana na umati uliopitiliza kumwagika barabarani! Pia kuna hii tour ya Burundi. Nyomi la hatari lilimwagika kupita mategeo ya waandaaji.



MISS KERI AMUOMBA MSAMAHA BEYONCE

Kutoka kwa producer mkali huko USA, Timberland, amesema kuwa 'Energy' hitmaker, Miss Keri yupo studio akitengeza ngoma kali iitwayo'Sorry' mahsusi kwaajili ya kumuomba radhi King Bey. Timberland amebreak the news kuwa kutokana na kutapakaa uvumi kuwa Miss Keri alimdiss Jay Z's wify basi sasa huu ni wakati muafaka wa kuanika kila kitu hadharani ili fans wa Keri na Bey wafahamu nini hasa kilitokea na yote hayo Keri ameelezea katika ngoma hiyo mpya ya 'Sorry'.

Just stay tuned kwasababu ngoma hii utaipata hapahapa!