Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Tuesday 21 January 2014

BEYONCE ATIMBA NA BLUE IVY IKULU YA OBAMA.

Kama Blue Ivy sio mtoto mwenye bahati zaidi duniani, je nani zaidi yake? Katika umri wa miaka 2 tu lakini ameshatia maguu ikulu ya Obama maarufuku kama White House. Ni  shamra shamra za miaka 50 ya kuzaliwa mke wa Barack Obama, Michelle Obama huko Washngton D.C.


Michelle Obama akiwa mpenzi na mshabiki wa kutupwa wa nyimbo za Beyonce ndipo hapo mke wa Jay Z na familia yake yote walipopata mwaliko. Kama kawaida Beyonce alipewa shavu la kupafomu na kama ilivyo ada, Beyonce hawezi kukuangusha linapokuja suala la kutoa burudani hasa wakiwepo watu wazito kama rais na familia yake. She never disappoints!


MWIGIZAJI THE ROCK AMZAWADIA BEKI 3 WAKE GARI LA THAMANI!

Ni mara ngapi unashukuru na kuthamini kile mtu anachokufanyia hata kama ni kidogo? Mwanamieleka wa zamani wa WWE na mwigizaji sinema za Fast and Furious, Dwayne Johnson a.k.a The Rock amemzawadia beki 3 wake gari aina ya Ford Edge, ambalo thamani yake ni zaidi ya dola za Kimarekani elfu 40. 

The Rock aliandika kwenye ukurasa wake wa Twitter, "Miaka 10 amekuwa akisaidia kazi za nyumbani kama mama yetu vile. Nimeamua kumpa surprise Esperanza na mkoko mpya #WeloveU" 

The Rock na beki 3 wake Espiranza