Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Tuesday, 29 January 2013

CHRIS BROWN AZICHAPA STUDIO


Jana Jumatatu Rihanna’s boyfriend Chris Brown alizichapa kavukavu dhidi ya Christopher Francis Ocean better known on stage as Frank Ocean. Brown alikuwa studio akimsikiliza mmoja wa wasanii wake na alipotaka kusepa ndipo alipokutana na Ocean akiwa na kundi lake. Ocean na wanae walikuwa wanamzuia Brown asiondoke huku Ocean akimwambia Brown kuwa hii ni studio yangu na umepaki gari lako katika sehemu yangu. 

Brown akaona isiwe ishu akasogea ampe mkono Ocean, Mara mmoja wa kundi la Ocean akamvamia Brown. Hapo ndipo Brown nae akalianzisha akipewa sapoti na washkaji zake pia!
Brown Vs Ocean
Mpaka polisi walifika eneo la tukio lakini Brown alikuwa ashasepa na Ocean alipohojiwa alisema kuwa chanzo ugomvi wao ni Brown kupaki katika eneo lake na kwamba Brown amemchapa makonde. 
Frank Ocean's twitter account
Frank Ocean ni singer pia mwandishi na ameshawaandikia mastaa kama Brandy, Justin Bieber, and John Legend.  

50 CENT: RICK ROSS AME-FAKE AJALI YAKE


Hatimaye rapper 50 Cent ameibuka na kumkashifu Rick Ross kuwa amefeki ajali aliyopata jana asubuhi wakati akitokea kwenye birthday party yake ambapo akiwa njiani alirushiwa risasi hivyo gari lake, Royce Rolls, kuhama njia na kugonga nyumba. Cent aliandika katika akaunti yake ya twitter, “Hahahaaaaaa Bonge amegonga nyumba? Inaonekana ni ishu ya kufoji.................................”

'Hahaha fat boy hit the building? Lol it looks staged to me, I ride like OBAMA level 6 bulet proof bomb proof, you already know. [sic]'


Ingawa 50 ameonyesha ku-dought tukio hilo lakini picha zinaonyesha wazi matobo ya risasi katika matairi, bampa na taa za gari la Ross. Ross na 50 wana bifu la muda mrefu toka 2009 Ross alipomchana Cent katika ngoma yake Mafia Music.

Gari ya Ross
Katika ajali hiyo hakuna aliyejeruhiwa katika gari alilokuwemo Ross, girlfriend wake Shateria L. Moragne na dereva wao. Japokuwa 50 ameonyesha mashaka lakini polisi wameichukulia ishu serious na bado wanaifanyia uchunguzi kwa sasa.

Ross
Ross, P Diddy, Fabolous Quincy Combs na Christina Milian

RICK ROSS ANUSURIKA KIFO


Alfajiri ya jana Jumatatu, The Miami based rapper William Roberts a.k,a Rick Ross alinusurika kuuawa baada ya gari lake kumiminiwa risasi na watu wasiojulikana. Ross alikuwa akitoka kwenye birthday party yake ya 37. Party hiyo ilihusisha list ndefu ya mastaa wakiwemo P Diddy, Fabolous Quincy Combs na Christina Milian just to mention a few.

Ross
Ross na Diddy
Ross, P Diddy, Fabolous Quincy Combs na Christina Milian
Rick Ross akiwa njiani huko Las Olas Boulevard baada ya kula bata usiku mzima, alianza kutupiwa risasi yeye akiwa ndani ya gari lake aina ya Rolls Royce ya silver isiyoingiza risasi! Katika sekeseke hilo dereva wa Ross alijikuta aligonga nyumba ya watu baada ya gari kupoteza mwelekeo.

 Hakuna mtu aliyejeruhiwa kutokana na taarifa ya polisi lakini inasemekana kuwa pengine bifu la muda mrefu lililopo kati yake na 50 Cent inaweza ikawa sababu.



Monday, 28 January 2013

NI WAKATI WA LULU KUTENGENEZA PESA?

Alifariki tarehe 7 April, 2012 na kuzikwa tarehe 10 April,2012. Ni miezi 9 imepita baada ya kifo cha mwigizaji maarufu Steven Charles Kanumba, The Great. Sababu au chanzo cha kifo chake kimekuwa bado kitendawili mpaka sasa huku kila mtu akijaribu kukisia sababu halisi. Baadhi ya media na hata polisi wamekuja na ripoti kuwa pengine unywaji uliopindukia wa kilevi cha whiskey, Jacky Daniels ndio sababu. Kuna waliosema eti Kanumba alikuwa mfuasi wa Freemasons ila alikiuka baadhi ya maagizo ndio ikapelekea kifo chake. Wengine wakasema kusukumwa na mwigizaji mwenzake Elizabeth Michael Kimemeta au Lulu ndio chanzo kufuatia majibizano kati yake na Kanumba wanaosemekana walikuwa wapenzi. Hii ikasababisha Lulu kukamatwa na kufunguliwa mashtaka ya ‘kuua’ na baadae ‘kuua bila ya kukusudia’. Lulu akatupwa rumande, tarehe 11 April, 2012.


Dhamana inayofikia milioni 40 imepitishwa na taratibu za kimahakama zimefuatwa hivyo Lulu  ametoka! Kifuatacho ni Lulu kugeuka kuwa lulu mbele ya media kwani vyombo vyote vya habari, ndani na nje vitamtafuta kwa ajili ya interviews. Sababu ni kuwa inaaminika Lulu pekee ndiye anayejua ukweli wa nini kilitokea usiku ule kabla ya umauti wa The Great!

Ni ukweli kuwa Lulu atakuwa bize sana kipindi hiki wakati kila media ikitaka story hiyo ya ndani ‘Exclusive’ ya kifo cha Kanumba. Je, Lulu ataweza kuendana na presha za media hizi? Je, ni wakati wa Lulu kupumzika kiakili na kimwili baada ya sekeseke hili, japo bado halijaisha!
Lulu ni lulu sasa! Ana mpango gani? Ameshafikiria tukio lake kuligeuza na kuwa bidhaa? Au yeye ataishia kulia na kupangusa machozi atakapokuwa anahojiwa na huku wengine wakiingiza pesa? Wakili wake pia ana mchango gani katika hili? Wazazi je?


Wapo waliojigeuza lulu kuendana na matukio na usupastaa wao mbele ya jamii. Mfano harusi ya Jay Dee na Gadner. Bang magazine pekee walipewa haki juu ya picha hizo. Huko South Africa kuna media ambayo tayari imeshanunua haki za kurusha kifo cha Mzee Nelson Mandela. Hayo ni baadhi tu ya matukio ambayo yaligeuzwa na mengine yataweza kugeuzwa kuwa bidhaa na kuingiza hela nyingi!