Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Monday, 6 May 2013

PAUL WA P-SQUARE AKATAA MTOTO WA PILI!

Katika kipindi kisichopungua mwezi mmoja, Paul Okoye amepata mtoto wa pili, tarehe 11 April demu wake wa siku nyingi, Anita alijifungua mtoto wa kiume, Andre Paul Okoye. Na sasa kuna taarifa zinasema kuwa demu wake mwingine, Elshama Benson Igbanoi, 19, amejifungua mtoto wa kiume huko Queen Charlotte and Chelsea Hospital, London na kupewa jina la Michelle Paul Okoye.
Michelle Paul Okoye
Chakushangaza Paul amemkataa mtoto huyo huku akiahidi kutua London ili kufanya DNA test kabla ya kukubali wajibu wake kwa mtoto kama baba. Baba wa binti huyo, Mzee Igbanoi amesema kuwa ameshamtumia e-mails za kutosha Paul toka binti yake akiwa mjamzito mpaka anajifungua lakini Paul hajajibu lolote.

Kuona hivyo Familia ya Mzee Igbanoi imeshafanya utaratibu wa kuwasiliana na Baba na Shangazi wa Paul huku akikazia kuwa binti yake hajawahi kuwa na mwanaume mwingine isipokuwa msanii huyo Paul Okoye ambaye ndiye alimtoa bikira Elshama akiwa na umri wa miaka 17.

Elshama
Mpaka sasa bado gharama za hospitali zinazozidi pauni 5,000 hazijalipwa na Elshama. Inasemekana kuwa Elshama ni rafiki pia wa Anita, msichana aliyemzalia huyuhuyu Paul Okoye mtoto wa kwanza tarehe 11 mwezi huu!

Paul Okoye na mtoto wake wa kwanza, Andre Okoye

Saturday, 4 May 2013

JUSTIN BIEBER ASIMAMISHA SHOW KUPISHA SWALA

Kipenzi cha walimbwende, Justin Bieber juzi Alhamiis alisimamisha show yake ili kupisha waumini wa dini ya Kiislamu kuswali (Waumini wa dini hiyo huswali mara tano kwa siku). Na baada ya swala dogo aliendeleza makamuzi kama kawaida. Hii ilitokea jijini Istanbul, Uturuki katika concert iliyofanyika Technical University sports arena.
Kupitia akaunti mbalimbali twitter za mashabiki wake walipendezeshwa na tukio hilo na kuandika hivi:-
Photo - Justin Bieber Stops Concert For Muslim Prayer
Pamoja na hayo bado Justin Bieber amekutana na vikwazo mbalimbali katika nchini za Kiarabu vikiwemo kufutwa kwa show yake huko Oman  kwa vile shows zake huchochea ngono kwa vijana!
 
 

JENGO LINALOFANANA NA UUME NCHINI CHINA.

Jengo hilo lenye urefu wa mita 150, hivi sasa bado linaendelea kujengwa jijini Beijing. Kutokana na muundo huo usiokua wa kawaida, picha za kibunifu zikaanza kuibuka katika website ambayo ni kama “Twitter ya China,” inayoitwa Sina Weibo.

Watu wengi wameeleza kuwa kwa kutumia ubunifu kidogo tu wa photoshopping, unaweza kuambatanisha picha ya jengo hilo, ambalo raia wamelipa nickname “Giant Penis” au “Uume mkubwa,” katikati ya “miguu” ya jengo lingine maarufu nchini humo ambalo ni makao makuu ya kituo cha TV cha China Central Television (CCTV,) almaarufu kama  “Big Underpants” building au Jengo la Chupi Kubwa.


Habari za utani huo zilifikia wakubwa nchini humo ambao walikerwa na kuamua kuwaharibia watu raha zao kwa kuamuru website ya Sino Weibo ku-block search zote zinazotafuta picha au habari za jengo hilo. Kwa sasa Wachina wakitafuta jengo hilo, wanakutana na ujumbe “kuendana na sheria, kanuni na sera husika, matokeo ya utafutaji wako (search results) hayawezi kuonyeshwa.


Mwandishi wa Reuters Anita Li amesema “hii inaonyesha frustrations miongoni mwa vijana watumiaji wa internet nchini China, na pia inaonyesha ni kiasi gani “wakubwa” wako sensitive kwa hata vitu vidogo vya kipuuzi online.”


Friday, 3 May 2013

RUGE MUTAHABA KUJIBU MAPIGO YA LADY JAY DEE!

Hatimaye mtuhumiwa namba moja kulingana na shutuma au tuhuma kadhaa alizokuwa akituhumiwa kwa takribani mwezi mmoja sasa na Lady Jay Dee, Mkurugenzi wa Clouds FM Ruge Mutahaba kwa mara ya kwanza atafungua mdomo wake siku ya Jumatatu asubuhi katika kipindi cha Power Breakfast ili kujibu tuhuma hizo!

Tayari mpaka sasa Jay Dee a.k.a Anakonda alishasema mambo kadha wa kadha akielekeza tuhuma kwa mmiliki Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba. Baadhi ya tuhuma za Lady Jay Dee kupitia akaunti yake ya twitter na blogspot yake ni kutopigwa nyimbo zake redioni Clouds Fm, kuingiliwa katika shows zake na hata kuwakataza baadhi ya wasanii hasa wale wa THT kutoshirikiana na Lady Jay Dee. 

Bifu lao hili limefika pabaya mpaka kufikia Jay Dee kutangaza kuwa hata akifa si Kusaga wala Ruge wasifike mazikoni na kuacha usia kuwa atakayewaona basi awatupie mawe!










BAADA YA KUUJAZA UWANJA, SASA WAPEWA JINA LA DR. CHAMELEON!

Hii haijawahi kutokea huko Uganda kwa local artistes. Show ya uzinduzi wa album ya ‘Badilisha’ ya Mfalme Doctor Chameleon iliyofanyika wiki iliyopita ndiyo mpaka sasa inayokamata namba moja kwa kuujaza uwanja huu wa Rugby, Kyaddondo Rugby grounds! Wamiliki wa huu uwanja wakaona isiwe tatizo, wakaamua kufuta jina la uwanja na sasa uwanja huu unaitwa Jose Chameleon Rugby grounds!

Siku ya show ya ‘Badilisha’, toka saa 10 jioni kulikuwa na foleni ya hatari ya raia na mpaka kufika saa 1 usiku, uwanja ulikuwa ushatema na watu elfu kumi walikuwa tayari wapo uwanjani kwa uzinduzi huo!

Bebe Cool the Prince ndio anafuata kwa kuujaza uwanja huo alipozindua albam yake ya ‘Kamwako’ na watatu ni The Novice Bobi kupitia albam yake ya ‘Tugambire Ku Jennifer’ ambapo aliingiza watu elfu 8.