Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Sunday, 17 February 2013

MARY J. BLIDGE AFILISIKA, MADENI KIBAO!


Kama unafikiri matatizo ya kufilisika kwa The Queen of Hiphop and Soul, Mary J. Blidge yamekwisha basi si kweli, mwanamama huyo ameingia katika msala mwingine wa kutakiwa kulipa kodi ya dola 900,000 huko New Jersey!

Hii ni baada ya mwanzoni mwa wiki iliyopita kushtakiwa kwa kuchelewa kulipa mkopo wa benki, dola 500,000. Ni mwaka uliopita tu Blidge alishtakiwa kwa kwa kutolipa mkopo wa benki wa dola milioni 2.2, na kabla ya hapo kituo chake kilishtakiwa pia kwa kosa hilohilo la kutolipa deni la dola 250,000.

Mary J. Blidge


RIHANNA AJA NA MAVAZI YAKE!

Baada ya kujijengea jina kubwa katika ulimwengu wa muziki duniani sasa Rihanna anaenda extra mile kwa kuingia rasmi katika tasnia ya ubunifu wa mavazi! Kwa mara ya kwanza this Barbadian singer aliingiza style mpya ya mavazi katika wiki ya mavazi huko London, London Fashion Week, jana Jumamosi!



The Stay singer alipata mapokezi mazuri toka kwa mashabiki na hata watu mashuhuri akiwemo Toni Jones aliye-comment kuwa mavazi hayo ‘yanavutia’ na ‘kuvalika’ pia!

Mavazi ya Rihanna yamelenga zaidi kuvaliwa na vijana na hasa ameanza na wa kike!











Angalia kipande kidogo cha video ya show hiyo:

Saturday, 16 February 2013

KIM KARDASHIAN ATUA NIGERIA, AUZA MJENGO WAKE!


The reality Tv star Kim Kardashian ametua nchini Nigeria saa moja lililopita. Kim K anayetarajia mtoto wake wa kwanza na rapper Kanye West yupo Nigeria kwa ajili ya ku co-host concert iitwayo ‘Love Like A Movie” ya Darey Art Alade, itakayofanyika kesho tarehe 17 February huko Eko Hotel Convention Center.


Kim alitua airport akiwa na bodyguard wake pamoja na makeup artiste
Wakati huohuo Kim ameuza mjengo wake uliomgharimu dola milioni 4.8 aliununua mwaka 2010. Inasemekana ameuuza kwa chini ya bei hiyo pamoja na samani za ndani kama makochi. Mjengo aliouuza alikuwa akiutumia yeye na x-boy friend wake, Kris Humphrey! 




Nje mpaka ndani ya mjengo alioupiga bei KK

DRAKE AZUIWA KUINGIA CLUB SABABU YA CHRIS BROWN!


Chris Brown na Drake sasa hawapikiki chungu kimoja! Usiku wa Jumatano Drake alizuiwa kuingia club moja sababu Chris Brown alikuwa tayari ndani!

Mabaunsa waliokuwa mlangoni klabuni Playhouse huko Hollywood walimkatalia katakata Drake kuzama ndani kula bata na wanae vile CB alikuwa tayari akila bata na washkaji zake katika party ya kampuni ya mavazi ya ‘Popular Demand’.
 
Mabaunsa walijuafika kuwa kama Drake angeingia ndani basi pengine kingetokea kilekile kilichotoka W.i.P. nightclub. Unakikumbuka? Majamaa walitupiana vyupa sana na kusababisa uharibika wakutosha!

Ki-gentleman, Drake alisepa zake kimyakimya bila kubishi!


EXCLUSIVE: MAPYA YA MAREHEMU GOLDIE: MUME WAKE AIBUKA NA USHAHIDI KIBAO WA PICHA ZA HARUSI YAO!