Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Saturday, 4 May 2013

JENGO LINALOFANANA NA UUME NCHINI CHINA.

Jengo hilo lenye urefu wa mita 150, hivi sasa bado linaendelea kujengwa jijini Beijing. Kutokana na muundo huo usiokua wa kawaida, picha za kibunifu zikaanza kuibuka katika website ambayo ni kama “Twitter ya China,” inayoitwa Sina Weibo.

Watu wengi wameeleza kuwa kwa kutumia ubunifu kidogo tu wa photoshopping, unaweza kuambatanisha picha ya jengo hilo, ambalo raia wamelipa nickname “Giant Penis” au “Uume mkubwa,” katikati ya “miguu” ya jengo lingine maarufu nchini humo ambalo ni makao makuu ya kituo cha TV cha China Central Television (CCTV,) almaarufu kama  “Big Underpants” building au Jengo la Chupi Kubwa.


Habari za utani huo zilifikia wakubwa nchini humo ambao walikerwa na kuamua kuwaharibia watu raha zao kwa kuamuru website ya Sino Weibo ku-block search zote zinazotafuta picha au habari za jengo hilo. Kwa sasa Wachina wakitafuta jengo hilo, wanakutana na ujumbe “kuendana na sheria, kanuni na sera husika, matokeo ya utafutaji wako (search results) hayawezi kuonyeshwa.


Mwandishi wa Reuters Anita Li amesema “hii inaonyesha frustrations miongoni mwa vijana watumiaji wa internet nchini China, na pia inaonyesha ni kiasi gani “wakubwa” wako sensitive kwa hata vitu vidogo vya kipuuzi online.”


Friday, 3 May 2013

RUGE MUTAHABA KUJIBU MAPIGO YA LADY JAY DEE!

Hatimaye mtuhumiwa namba moja kulingana na shutuma au tuhuma kadhaa alizokuwa akituhumiwa kwa takribani mwezi mmoja sasa na Lady Jay Dee, Mkurugenzi wa Clouds FM Ruge Mutahaba kwa mara ya kwanza atafungua mdomo wake siku ya Jumatatu asubuhi katika kipindi cha Power Breakfast ili kujibu tuhuma hizo!

Tayari mpaka sasa Jay Dee a.k.a Anakonda alishasema mambo kadha wa kadha akielekeza tuhuma kwa mmiliki Joseph Kusaga na Ruge Mutahaba. Baadhi ya tuhuma za Lady Jay Dee kupitia akaunti yake ya twitter na blogspot yake ni kutopigwa nyimbo zake redioni Clouds Fm, kuingiliwa katika shows zake na hata kuwakataza baadhi ya wasanii hasa wale wa THT kutoshirikiana na Lady Jay Dee. 

Bifu lao hili limefika pabaya mpaka kufikia Jay Dee kutangaza kuwa hata akifa si Kusaga wala Ruge wasifike mazikoni na kuacha usia kuwa atakayewaona basi awatupie mawe!










BAADA YA KUUJAZA UWANJA, SASA WAPEWA JINA LA DR. CHAMELEON!

Hii haijawahi kutokea huko Uganda kwa local artistes. Show ya uzinduzi wa album ya ‘Badilisha’ ya Mfalme Doctor Chameleon iliyofanyika wiki iliyopita ndiyo mpaka sasa inayokamata namba moja kwa kuujaza uwanja huu wa Rugby, Kyaddondo Rugby grounds! Wamiliki wa huu uwanja wakaona isiwe tatizo, wakaamua kufuta jina la uwanja na sasa uwanja huu unaitwa Jose Chameleon Rugby grounds!

Siku ya show ya ‘Badilisha’, toka saa 10 jioni kulikuwa na foleni ya hatari ya raia na mpaka kufika saa 1 usiku, uwanja ulikuwa ushatema na watu elfu kumi walikuwa tayari wapo uwanjani kwa uzinduzi huo!

Bebe Cool the Prince ndio anafuata kwa kuujaza uwanja huo alipozindua albam yake ya ‘Kamwako’ na watatu ni The Novice Bobi kupitia albam yake ya ‘Tugambire Ku Jennifer’ ambapo aliingiza watu elfu 8.


Thursday, 25 April 2013

NDANI YA MJENGO WA PETER P-SQUARE!

Muda mfupi uliopita Peter Okoye ametupia picha zifuatazo kwenye page yake ya Instagram na kuandika, "home sweet home".






 

 


T-PAIN ANYOA DREADS!

Msanii wa Hip-hop na RnB pande za USA, T-Pain, ameamua kunyoa dreads zake. T-Pain pia aliandia hivi kupitia instagram, "We must all learn to adjust with our surroundings. Those who get stuck doing the same things for too long are bound to get left behind the strong who press on and reinvent themselves. Also. Good news. Hair grows back,"

T-Pain wa zamani
T-Pain pia alichukua nafasi kutangaza ujio wake mpya wa albam, 'Stoicville' bila kutaja lini itakuwa tayari but just tay tuned!
T-Pain mpya