Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Monday, 18 March 2013

P-SQUARE WAISIMAMISHA MALAWI!

The Alingo stars, P-Square wako katika tour yao katika mataifa ya barani Afrika na wik-end iliyokwisha walikuwa nchini Malawi na kuangusha bonge moja la show. Show ilikuwa hivi:








JUMBA BEI GHALI ZAIDI NCHINI UINGEREZA!

Hii ndio nyumba ghali nchini Uingereza. Kutokana na bei yake kuwa juu sana ilibidi ipunguzwe kwa takribani pauni milioni 35. Na hii imechukua miaka miwili bila mnunuzi kupatikana.  Na sasa bei yake ni pauni milioni 65 tu!


Bangaloo hili lina vyumba 14 vya kulala na linapatikana katika mtaa wa Hampstead, mtaa huu unajulikana kama 'Billionaires' row' kwa sababu wakazi wa eneo hilo ni wanauwezo kiuchumi!



 Jumba hili la kifahari lilijengwa mwaka 1910 liliwekwa sokoni toka mwaka 2011 na bei yake ilikuwa ni pauni za Uingereza, milioni 100.






















Sunday, 17 March 2013

PETER MSECHU KUZALIWA UPYA KESHO!

Peter Msechu kesho atasherehekea siku yake ya kuzaliwa kwa kutimiza miaka kadhaa. Peter Msechu ambaye ni Bongo Star Search na Tusker Project Fame Star anatarajia pia ku-release his new hit single hiyo kesho. 

Ngoma hiyo inaitwa 'Kumbe' amemshirikisha 'Mwamba wa Kaskazini', Joh Makin!   

Happy Birthday Peter Msechu.




Saturday, 16 March 2013

ALINGO Vs AZONTO

Kumeibuka ghasia na kutupiana kwa maneno katika mitandao ya jamii baina ya Wanigeria na Waghana kuhusiana na styles hizi mbili za Alingo na Azonto. Na sokomoko hili limekuja hasa baada ya artiste wa dancehall toka Ghana, Samini kutoa ngoma kwa kutumia biti ya Alingo kuwadis P-Squae kwa kukopi dance ya Azonto na kuitumia katika Alingo!

 Wewe unafikiri style ipi ya ku-dance ni kali kati ya ile ya Azonto na Alingo? Na je, ni kweli styles hizi zinafanana?















































LIL WAYNE BADO YUPO HOI HOSPITALI!

Young Money Cash Money brother, Lil Wayne alikimbizwa hospitali hivi majuzi baada ya kuzidiwa. Hali yake ilikuwa mbaya sana kiasi cha kukutwa akiwa sakafuni chumbani kwake hajitambui. Mpaka sasa hali ya Wayne si nzuri sana licha ya ku-tweet kuwa yupo poa!


Ndugu, jamaa, marafiki na rap artistes kadhaa walimiminika hospitalini siku ya Jumatano kumjulia hali Wayne. Hali hii ya Lil Wayne inatokana na ubwiaji unga aina ya codeine uliopitiliza. Inasemekana madaktari walikuta kiasi kikubwa cha madawa hayo mwilini mwa Wayne hivyo kupelekea madaktari kuamua kuusafisha mwili wa Wayne mara tatu.

Pamoja na hayo yote jana Ijumaa Lil wayne aliibuka na ku-tweet kuwa yupo fresh na kuwashukuru fans wake kwa sala zao na upendo kwake!