Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Thursday, 7 March 2013

CHRIS BROWN AMTIMUA KAZI BAUNSA WAKE WAKIWA AIRPORT!

Baada ya kugonga show kali huko Ghana juzi tarehe 5 Accra Sports Stadium, 'Don't Wake Me Up' singer Chris Brown na crew yake wakala flight mpaka Bermuda huko Caribbean Island Jumatano (06.03.13). Wakiwa bado hawajatua ndipo kukatokea mtiti kati ya Brown na baunsa wake wa muda mrefu Big Pat! Inasemekana walichapana makonde. 


Walipotua Bermuda ndipo Brown akamwambia Big asikwee tena ndege yake aliyoikodi. Na huo ndio ukawa mwisho wa uhusiano wa kikazi kati yao na ilibidi Big Pat achukue ndege nyingine mpaka New York City's JFK Airport.



Tuesday, 5 March 2013

JUSTIN BIEBER KAMA MZALAMU VILE!

Justin Bieber amewaomba radhi mashabiki wake kwa kuchelewa kupafomu katika show yake huko London kwa dakika 40, jana usiku!


Mashabiki wengi vijana, watoto pamoja na wazazi wao waliondoka ukumbini O2 Arena wakiwa wamejawa na hasira na gadhabu kwa kutomwona JB! Bierber alijitetea baadae kuwa alichelewa kupiga show kutokana na matatizo ya kiufundi na hajachelewa kuanza show kwa masaa 2 kama ilivyodaiwa!
Viti vingi vikiwa tupu baada ya kundi kubwa la mashabiki wa Bieber kuondoka







2FACE KUFUNGA NDOA MWEZI HUU!

Kama kuna tukio kubwa na la kusisimua linalosubiriwa kwa hamu kubwa nchini Nigeria na Afrika basi ni hili la ndoa ya 2face Idibia na Annie Macaulay. Japokuwa 2face na Annie tayari ni mme na mke kisheria lakini bado kuna ndoa ya kimila na ile ya kanisani. 

Invitation Card
Tarehe 8 Machi ndio imepangwa rasmi kufanyika ndoa ya kimila huko Nigeria Mashariki (nyumbani kwa Annie) na ile ya kanisani itafuata tarehe 23, Machi huko Dubai!

And it is strictly for invite!

Gauni la Annie limedizainiwa na Vonne Couture!



Monday, 4 March 2013

DRAKE AMWAGA MVUA YA DOLA CLUB!

Zaidi ya dolari 50,000 zilimwagwa kama mvua kwa mademu wacheza uchi, stippers na The Canadian born rapper Drake ndani ya Cameo Night Club huko Charlotte jana usiku! Drake alipomaliza mvua ya mkwanja huo floor nzima ilifunikwa kwa mihela hiyo ya Kimarekani.

Drake alizama club na mkwanja huo ukiwa ndani ya box moja kabla ya ku-make rain full of money.






Rapper mwingine Bleu Davinci aliendeleza mvua hiyo kwa kumwaga zaidi ya dola 25,000  




Thursday, 28 February 2013

SCHWARZENEGGER APATA DAKTARI WA MOYO WAKE!

Terminator, Arnold Schwarzenegger yuko katika mikono salama sasa. Ipo hivyo kwa sababu demu wake mpya ni daktari bingwa! Anaitwa Heather, na kwa mara ya kwanza walionekana katika dinner date huko Santa Monica!



Vyanzo vya udakuzi vinasema kuwa Heather sio dokta wa kawaida tu vile alishawatibu watu wazito mbalimbali akiwemo mkimbiaji maarufu, George St-Pierre. So haijajulikana kama Heather anamtibia Schwarzenegger na ni kwa ugonjwa upi! Infact she is not in the normal group of people who treat Governator, Schwarzenegger.

We smell romance.....