Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Friday, 23 August 2013

SKETI YAMVUKA TONI BRAXTON STEJINI!

Mwanzomi mwa wiki hii huko New Jersey, mama wa watoto wawili, mwanamuziki Toni Braxton aliwapa mashabiki wake zaidi ya kile walichokilipia kwaajili ya show hiyo. Wakati akiwa stejini akipiga show hiyo Toni Braxton, 42, alishangaa akiona sketi yake nyepesi ya metallic akimvuka na kuacha makalio yake wazi!




Kwa bahati mbaya Toni Braxton hakugundua kuwa sketi yake imemvuka kwani aligeuka na kuwapa mashabiki mgongo huku akitingisha makalio yake kwa mbwembwe asijue kinachoendelea kumbe ndio anawamwagia utamu huku mashabiki wakilipuka kwa shangwe la hatari!



Toni Braxton aliendelea na show mpaka jamaa mmoja alipokwea stejini na kumfunika kwa koti la suti yake.



Thursday, 22 August 2013

DIAMOND KULA MKWANJA MREFU KWA KUFANYA COLLABO KENYA

Mshindi wa tuzo ya mwimbaji bora wa Gospel nchini Kenya, Willy Paul ametangaza kupiga kolabo na msanii mwenye kukamata headlines kila uchao Bongo na nje ya Tanzania, Diamond Platinumz! Willy alikutana na Diamond katika concert moja iliyohappen huko Nairobi Ijumaa iliyopita.

"Diamond alivutiwa sana na kazi zangu kama mimi kwa kazi zake. Nafahamu anachaji pesa so nitamsikiliza anahitaji kiasi gani na nipo radhi kumpa mkwanja autakao". 


.


BRANDY AGOMA KUPIGIA SHOW VITI!

Mwanadada Brandy hakuwa na siku nzuri siku ya Jumamosi iliyopita baada ya kupiga show kwa watu 40 tu kati ya mashabiki 90,000 waliotakiwa kuingia katika show hiyo. Hii ilitokea hapo kwa Madiba, katika uwanja wa FNB stadium, Afrika Kusini katika siku maalum ya 'Mandela Sports and Culture day'. 

Tatizo lilitokea ni kuwa mapromota wa event hiyo hawakuwataarifu watu waliohudhuria shughuli hizo kwani baada ya shamrashamra za hapa na pale raia wakaondoka wakijua shughuli imeisha kumbe Brandy aliwekwa kama 'surprise artist '. Ndipo hapo sasa mwanadada huyo alipopanda stejini na kuwaimbia watu wasiopungua 40 tu huku viti zaidi ya 80,000 vikiwa tupu! Baada ya kupafomu ngoma mbili tu Brandy aliacha steji na kusepa zake!


STAR WA PRISON BREAK AJITANGAZA NI SHOGA!

Starring wa tamthiliya ya Prison Break, Wentworth Miller a.k.a Michael Scofield ametangaza jana Jumatano kuwa yeye ni shoga. Amefanya uamuzi huu baada ya kukataa mwaliko wa kuhudhuria sherehe za jumuiya ya wanafilamu katika mchakato wa kukataa au kupinga 'ushoga' nchinu Urusi.


Baada ya Michael Scofield kupokea mwaliko huo uliopewa jina la St. Petersburg International Film Festival, alisema, "Mimi kama shoga ni lazima nikatae". Scofield aliendelea kusema, "Nachukizwa na vile jinsi mashoga na wasagaji wanavyochukuliwa na serikali ya Urusi. Kwahivyo siwezi kushiriki katika kampeni hii ambapo watu kama mimi hawapewi haki zao za msingi"


Tuesday, 20 August 2013

BOBI WINE AMCHANA BEBE COOL!


Ni muda sasa umepita tangu bifu la Bobi Wine na Bebe Cool lianze na sio kwamba linaelekea kufifia au kufa, la, bado mafahali hawa wawili hawaivi chungu kimoja! Na juzi tu Bobi Wine alikuwa na haya kumwambia Bebe Cool.
 

"Sina tatizo lolote na Bebe Cool lakini ana matatizo na yeye mwenyewe, ni kama vile watoto wadogo wakati mnakua. Wengine hukua na kupevuka haraka na wengine hubaki nyuma kama yeye ila sitaki anirudishe nyuma. Ni kama vile niliponunua ndege yangu, yeye hupenda kuzungumzia vitu vyangu kwa vile nam-inspire, inafurahisha sana"