Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Monday, 10 June 2013

RIHANNA AVUNJA REKODI UFARANSA

Haijawahi kutokea! Katika umri wa miaka 25 tu, Rihanna ameweza kuweka historia kwa kuujaza uwanja wa kandanda wa Stade De France alipogonga show yake ya wazi Week-end hii. Ni Lady Gaga pekee ndio aliyekuwa ameishikilia rekodi hiyo kwa kuutitirisha uwanja huo akiwa na umri mdogo, miaka 26 lakini Rihanna amemfunika vibaya Lady Gaga huku Rihanna akiwa ana miaka 25 tu.


Mmoja kati ya fans wake ali-tweet hivi baada ya show hiyo:
"Rihanna is also the youngest person to ever headline Stade De France"




CHRIS BROWN MAHAKAMANI LEO

The bad boy Chris Brown anatarajiwa kukutana uso kwa uso na pilato leo hii mezani kukiwa na mashtaka yanayomkabili kwamba hakukamilisha muda rasmi aliotakiwa kuitumikia jamii (community service), ikiwa kama adhabu baada ya kukutwa na hatia ya kumchapa makonde aliyekuwa girlfriend wake, Rihanna, mwaka 2009. Chriss Brown alitakiwa aitumikie jamii kwa siku 180 na April mwaka huu alikuwa mahakama lakini pilato aliihairisha kesi hiyo baada ya kukosa baadhi ya taarifa muhimu.


Chris Brown yupo mbioni kutoa albam yake ya 6 iitwayo "X", tarehe 16, July akiwashirikisha Kendrick Lamar, Nicki Minaj, Wiz Khalifa na Jennifer Lopez na tayari ameshatanguliza ngoma ya 'Fine China" ambayo ipo namba 31 katika Billboard Hot 100 chart. 


KANYE WEST ASHEREHEKEA BIRTHDAY BILA KIM KARDASHIAN

Kanye West ametimiza miaka 36 na kuangusha bonge la party la kimya kimya. Party hili liliwahusisha watu wake karibu tu wakiwemo Beyonce na Jay Z. Nas pia alikuwepo mjengoni. Ila kilichowashangaza watu wengi ni kutoonekana kwa mama kijacho wake, Kim Kardashin. 


Lakini wataalam wa mambo wanasema kuwa Kim K alishindwa kupaa mpaka New York kwavile yupo katika nyakati za majeruhi akikaribia kabisa siku zake za kumleta duniani mtoto wake wa kwanza ambaye tayari madaktari wameshasema kuwa atakuwa mwenye jinsia ya kike! 


Friday, 7 June 2013

NAZIZI AMWANIKA MTOTO WAKE!

Nazizi, rapper toka Kenya wa crew ya Necessary Noise amemwanika mtoto wake wa kiume anaitwa Tafari  huko Nai! Nonini ameonekana akiwa na Tafari muda mwingi na hasa hivi majuzi alipokuwa na katika breakfast show, OneFm. 


Mwaka huu Tafari anatimiza miaka 3 na anaoneka he is just like his mother kwa swaga zake.



Wednesday, 5 June 2013

MR NICE ATEMWA GRANDPA RECORDS, KENYA.

Baada ya kufulia kimuziki achilia mbali maisha, star wa 'Kikulacho' toka nchini Tanzania aliamua kuhamishia shughuli zake za kimuziki nchini Kenya. Na huko Kenya alidaka dili la kusaini mkataba na GrandPa records na kufanikiwa kurekodi ngoma kadhaa. Miezi miwili sasa imeshapita toka alambe mchongo huo lakini hii leo the CEO wa kampuni GrandPa records, Refigah aliitisha press conference na kutangaza kumtema Mr. Nice.


Refigah alieleza sababu za kumwaga Mr. Nice ni pamoja na uzembe wa msanii, kutokuwa mshindani kimuziki na msanii mwenewe kutoheshimu mkataba huku ikisemekana kuwa kumbe Mr. Nice alikuwa na mkataba na record label nyingine huku Tanzania angali amesaini na GrandPa records.