Unaambiwa hajawahi kutokea msanii mwenye kutunza siri huko Naija
kama Geneveive Nnaji. Geneveive ameweza kumficha binti yake kwa kipindi kirefu
sana bila media yoyote kushtukia. Kwasasa binti yake anatimiza miaka 18 ndio
kama media wanasanuka hivi.
Geneveive alipata ujauzito akiwa na miaka 15 tu. Mpaka sasa
hajafahamika baba wa mtoto huyo ni nani lakini mchizi mmoja
anayeitwa Acura amejitokeza na kudai yeye ndio mshua wa binti huyo!
The
exclusive pictures unazoziona ni huyo binti yake Geneveive, Chimebuka a.k.a
Lily akiwa zake huko Ughaibuni akimalizia high school na inasemekana modelling
ndio ndoto yake!
Huyu ni
msanii wa nchini Uganda. Akiwa on stage bila hiana wala kubana aliwaachia
mashabiki wake wafanye chochote watakacho pale aliwasogelea na kuwaachia sehemu
zake za siri. Baadhi ya mashabiki waliingiza mikono yao kunako nyeti za msanii
huyo bila hata yeye kushtuka wala kujinasua toka kwa mashabiki hao waliokuwa
wana uchu!
Alikuwa moto kwelikweli at his times, Afrika Mashariki na Kati. Mr. Nice, mwimbaji wa ngoma kama ‘Kikulacho’ iliyomfanya avute mkwanja mrefu pengine kuliko msanii mwingine yeyote kwa wakati wote hapa Tanzania. Baada ya kupiga shows lukuki nje na ndani ya Tanzania Mr. Nice alianza kudrop taratibu na katika press conference yake leo hii alisema sababu yeye kushuka ilikuwa ni management yake.
Mr. Nice pia alikanusha kuwahi kuwa na bifu na Jose Chameleone wa Uganda. Zaidi ya hapo Mr. Nice alizungumzia kuhusu wimbo wa “Mac Muga” wa Ali Kiba kuwa haukuwa ukimuhusu yeye na maisha yake ya kimuziki, yaani kupanda na kuporomoka kwake! Mr. Nice alikana kuwa alikwenda Afrika Kusini, hali ya kimisha ikawa mbaya mpaka kurudishwa nyumbani Tanzania. Mr. Nice alikana kwenda Afrika Kusini na kusema kuwa Ali kIba hajawahi hata siku moja kusema kuwa ngoma hiyo inamuhusu yeye Mr. Nice!
The King is back. Mr. Nice amerudi upya katika game na this time amemshirikisha DNA toka Kenya, ngoma inaitwa ‘Tafuta’. Mr. Nice ame-sign label deal na Grandpa production ya Kenya na tarehe 26 April ataanza mfululizo wa kugonga shows hukohuko KE.
Gwiji la muziki nchini Tanzania hususan taarab asilia, Fatuma Binti
Baraka "Bi Kidude" hatunaye tena. Taarifa kutoka katika familia yake
zinasema Bi Kidude alikuwa akipatiwa matibabu katika hospitali ya Hindu Mandal
amefariki leo. Bi Kidude atakumbukwa kama mwanamuziki mkongwe zaidi nchini
ambaye alianza muziki akiwa na umri wa miaka 10 tu na aliwahi kupokea tuzo
mbalimbali kutokana na mchango wake katika muziki wa mahadhi ya mwambao. Hakika
sanaa nchini imepoteza moja ya nguzo kubwa.