Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Friday, 17 August 2012

NGOMA MPYA YA TIP TOP CONNECTION - RIZIKI

PAH ONE NA CAMP MULLA WANAUFANANO

Japo si haki kuyalinganisha makundi haya kwa kuzingatia mafanikio na umaarufu kutokana na ukweli kwamba Camp Mulla wapo mbali zaidi na wanajulikana kimataifa kuliko Pah One, kuna mengi yakufanana katika makundi haya mawili. Cha kufurahisha zaidi ni kuwa yote ni coincidence tu na hakuna lililoiga kundi jingine. Pah One wanawakilisha Tanzania na Camp Mulla wanawakilisha Kenya. 


Haya ni mambo kumi wanayofanana:

1. Makundi yote  yaliundwa miaka miwili ama mitatu iliyopita

2.Makundi yao yanaundwa na waimbaji/marapper wanne

PahOne – Aika, Ola, Nah Reel na Igwe

Camp Mulla - Taio Tripper, Shappa Man, Miss Karun, K'Cous , Japo yupo pia
Mykie Tuch ambaye ni CEO

Camp Mulla
3.Kila kundi lina wavulana watatu na msichana mmoja

PahOne – Aika

CampMulla -  Miss Karun

4. Kila kundi lina producer ambaye ni member pia na nyimbo zao hutengeneza wenyewe

PahOne – Nah Reel
Camp Mulla - K'Cous na Shappa Man


5. Wengi wana miaka chini ya 25

6. Wengi bado wanasoma

7. Karibu wote wanatokea kwenye familia bora
Pah One – Ola na Igwe wamesomea Afrika Kusini , Aika na Nah Reel wamesomea India

Camp Mulla – Mtandao mmoja uliwahi kuwaponda kuwa wanapendelewa kwakuwa wanatoka kwenye familia bora

Pah One
8. Muziki wanaofanya ni wa aina moja (Hip hop, dance na aina zingine za muziki wa kisasa)

9. Uvaaji wao unafanana sana

10. Wote wana akaunti maarufu ya mtandao wa muziki wa Reverbnation

KEKO KUKINUKISHA JIJINI MWANZA WEEKEND HII

 
 
Rapper wa kike toka nchini Uganda, Keko anatarajiwa kupiga show weekend hii jijini Mwanza.
 
Taarifa hiyo ameitoa mwenyewe kupitia Twitter account yake.

“TANZANIA ARE YOU READY!!! #KEKONIANS IN MWANZA #MAKEYOUDANCE COMING TO YOU THIS WEEKEND tell every & anyone KEKO Coming!!”

Hata hivyo mpaka sasa haijawa wazi ni nani anayempeleka jijini humo ama show itafanyika wapi kwakuwa hakuna matangazo yaliyotolewa.

THE MAKING OF BAADAE-OMMY DIMPOZ

KOFFI OLOMIDE ATUPWA JELA MIAKA MITATU


Stori kutoka Kinshasa Congo DRC zimetoa uthibitisho kwamba mwanamuziki maarufu ambae jina lake lina uzito ndani na nje ya Afrika, Koffi Olomide, amehukumiwa kwenda jela kwa miaka mitatu au kulipa faini.
Kilichomfanya star huyu wa rhumba mwenye miaka 56 apigwe nyundo hizo ni fujo alizozifanya akiwa kwenye hoteli moja maarufu Congo DRC pamoja na kumpiga meneja wake kwa jina la Diego Lubaki.
Nimemsikia mwandishi wa DW kutoka Congo akisema Koffi alikua akitetewa na zaidi ya mawakili 15 ambapo mamia ya mashabiki wake walihudhuria Mahakamani kusikiliza kitatokea nini kwenye kesi yake August 16, 2012.Kabla ya kufikishwa Mahakamani Koffi alikamatwa na polisi August 15 jioni muda mfupi tu baada ya kufanya fujo hizo na kuwekwa kwenye rumande ya mahakama ndogo Kinshasa kutokana na makosa aliyofanya hotelini ikiwa ni pamoja na kumpiga meneja wake ambae amekua akiishi Ulaya.
Mwandishi wa DW amesema ugomvi huo umetokana na Koffi kumdai meneja huyo euro elfu sita ambapo mashahidi kwenye eneo la tukio wamekiri kwamba Koffi alimpiga ngumi meneja wake pamoja na kuvunja mlango wa hoteli.
Hata hivyo meneja huyo aliwasilisha Mahakamani hoja ya kuondoa mashtaka yake dhidi ya Koffi na kupendekeza kuwepo kwa maridhiano kati yao lakini majaji walilipiga chini hilo ombi lake.
Baadhi ya wananchi waliotoa maoni kuhusu hiyo kesi ya Koffi wameunga mkono adhabu hiyo na kusema amezidisha, Ulaya ni yeye na kwengine ni yeye, mwingine amesema ni safi kwa sababu hii sio mara ya kwanza kwa yeye kutenda kosa.
Kutokana na adhabu hiyo kiongozi wa mawakili wanaomtetea Koffi amesema wamepanga kukata rufaa lakini wanasubiri maoni ya Koffi mwenyewe.…