Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Wednesday 20 February 2013

OSCAR PISTORIUS ASHIKWA PABAYA MAHAKAMANI!

Ile kesi ya Oscar Pistorius, mkimbiaji riadha kwa kutumia miguu ya bandia, kutuhumiwa kumuuwa mpenzi wake Reeva Steenkamp siku ya Valentine imepata taswira mpya leo hii! Shahidi mmoja akitoa ushuhuda wake mahakamani jana alisema kuwa Oscar Pistorius alipomtungua  Reeva kwa bastola yake kwa maya ya kwanza, Reeva alisikika akilia, lakini Pistorius aliendelea kummiminia na kummiminia risasi!

Pistorius mahakamani

Oscar Pistorius na Reeva Steenkamp
Ikiwa bado masikilizano ya dhamani yakiendelea siku ya Jumatano shahidi mwingine alisema kuwa alisikia mlio wa risasi huku kukiwa na mwanga, mara akasikia mwanamke akilia kwa maumivu, na tena milio ya risasi iliendelea. Sasa hii ni tofauti na maelezo ya Pistorius aliyesema mahakamani kuwa alimpiga mtu (mpenzi wake) kukiwa na giza nene. Zaidi ya hapo bado upande mashtaka unasema kuwa upo ushahidi wa kuwepo kwa majibizano baina ya Pistoruis na Reeva kati ya saa nane na tisa usiku kabla ya mauaji.

Chooni ulipokutwa mwili wa marehemu Reeva Steenkamp
  
Ushahidi huu wote unamuweka Pistorius katika wakati mgumu zaidi hasa wa kupata dhamani kwa wakati huu.



No comments:

Post a Comment