Tanzania top model audition

Tanzania top model audition
Tanzania top model audition

Monday, 20 May 2013

JCB AFUNGA PINGU ZA MAISHA NA MZUNGU!

Mwanahip-hop toka A-Town, 'Ukiskia paah' hitmaker single, JCB ameachana na ukapera this week-end kwa kufunga ndoa. Na hizi ni baadhi ya picha za harusi hiyo iliyofanyika Arusha Jumamosi hii!



 

SIKILIZA HOTUBA YA SUGU ILIYOSABABISHA BUNGE KUHAIRISHWA LEO HII!


Friday, 17 May 2013

MNYAMA AMPOTEZEA ANACONDA

TID a.k.a Mnyama amemtema au amemtolea nje Lady Jay Dee a.k.a anaconda kushiriki katika show yake ya kutimiza miaka 13 katika mziki pale Nyumbani Lounge mwishoni mwa mwezi huu. Hii inakuja baada ya Jay Dee kuingia katika mzozo mkubwa na Mkurugenzi utafiti wa redio binafsi, Clouds Fm, Ruge Mutahaba!
 
Katika kuthibitisha kwake kutoshiriki show hiyo, TID aliandika hivi katika ukurasa wake wa facebook:-
“Three reasons why I can’t do Lady Jay Dee Show….. No 1 I have better contract which pays me better than. No 2 I really don’t want to be between anybody’s conflict, ya kwangu yananishinda naona niepushe shari. No3 nataka kuoa muda wangu ndio huu………. Kama nimekukosea captein na madame kazeni but I have been tru the same shit”
 
TID anaungana na wasanii kama Linah, Barnaba na Matonya ambao walishatangaza hapo wali kuwa hawatashiriki kabisa katika show hiyo. Amebaki Professor Jay.
 
 

Thursday, 16 May 2013

D' BANJ ALA SAHANI MOJA NA BARNABA BOY

Wakati wasanii wa Kibongo wakihaha kutafuta michongo mbalimbali ya kuwaingiza mkwanja ikiwemo kupata haki sahihi ya umiliki wa ringtones zao na zaidi kupata mashavu ya kuwa mabalozi wa makampuni mbalimbali, huko kwa wenzetu hasa West Africa wameshapiga hatua kubwa sana katika hili.

Achilia mbali tuzo lukuki na hits anazozidondosha siku baada ya siku, neema zinaonekana bado kumdondokea artiste huyu kwani leo hii KokoMaster a.k.a D’ Banj alisaini mkataba wa kuwa balozi wa benki moja huko Naija iitwayo Bank of Industry.
Ms Evelyn Oputu, Managing Director & Chief Executive Officer of Bank of Industry na balozi D' Banj


 
Hapa Tanzania hii imekuwa hatua mpya sasa hasa kwa upande wa mabenki kuwachagua wasanii wazawa kuwa mabalozi wake na mfano hai tu ambao kidogo unaendaana na huo wa msanii kuwa balozi ni wa Barbana Boy kufanya kazi na benki ya Barclays Tanzania (japo Barnabas si balozi wa benki hiyo) lakini cha msingi ni lile dili tu kati yake na benki hiyo ambapo Barnabas ataingiza zaidi ya dola za Kimarekani 20,000/=kwa kuimba wimbo juu ya wanawake wa Kitanzania.